[Latest Updates]: Waziri Mavunde Ataka Wizara na Taasisi Kuendeleza Utamaduni wa Michezo ya Pamoja

Tarehe : June 28, 2025, 2:37 p.m.
left

Asisitiza umoja na mshikamano

Eng.Samamba asema Bonanza limelenga kumarisha afya, kujenga mshikamano 

Dodoma
Waziri wa Madini  Mhe.Anthony Mavunde  amewataka Watumishi wa Wizara na taasisi zake kuendeleza  utamaduni wa kufanya michezo ya pamoja na kueleza kuwa  inasaidia kuimarisha afya na  utendaji kazi za Wizara.

Ameyasema hayo leo Juni 28, 2025 wakati akifungua Bonanza la Wizara ya  Madini na Taasisi zake lililofanyika katika Viwanja vya Shule Sekondari John Merlin, jijini Dodoma.

Ameongeza kuwa, Sekta ya Madini imeendelea kufanya vizuri  katika maeneo mbalimbali ikiwemo mchango wake kwenye Pato la Taifa na kutumia nafasi hiyo kumshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutokana na maelekezo na miongozo  yake  ambayo inaifanya Sekta kuendelea  kupiga hatua.

Pia, amemshukuru Katibu Mkuu Wizara ya Madini Eng.Yahya Samamba 
kwa ushirikiano wake na kuendeleza michezo ya pamoja suala ambalo linachochea umoja miongoni mwa watumishi na kuongeza tija kwenye kazi.

"Nawashukuru sana watumishi wa Wizara na taasisi zake katika kipindi changu cha miaka miwili kasoro ndani ya Wizara sote tumefanya vizuri. Hata jana Mhe. Rais alipofunga Bunge alizungumzia kuhusu Sekta ya Madini kuendelea kufanya vizuri.Sifa huwa zinarudi kwetu lakini ninyi ndiyo wafanyakazi," amesema Mavunde.

Amesisitiza kuhusu watumishi kuendelea kufanya kazi kwa bidii ikizingatiwa kwamba Mwaka wa Fedha 2025/26 Wizara imewekwa malengo makubwa  ambayo yanapaswa kutekelezwa kwa manufaa ya taifa kiuchumi.

"Tuendelee tuliposhia ili Sekta itoe mchango zaidi na siku moja iwe Sekta kinara kiuchumi nchini," amesema Waziri Mavunde.

Akizungumza katika bonanza hilo, Katibu Mkuu Wizara ya Madini Eng. Yahya Samamba amesema kwamba kufanyika kwa bonanza hilo ni utekelezaji wa maelekezo ya Waziri Mavunde ambaye kipindi ameteuliwa kuingoza Wizara aliomba Wizara watumishi wa Wizara na taasisi kukutana pamoja kupitia  michezo ili kujenga umoja na ushirikiano miongoni mwa watumishi.

Naye, Kamishna wa Madini Dkt. Abdul Rahman Mwanga amempongeza Waziri Mavunde  kwa kuisimamia Sekta vizuri  na kusema, "ni matamanio yangu  upite na urudi tena kuendeleza tulipoishia,".

Bonanza hilo limeaongozwa na kaulimbiu isemayo

Michezo ni furaha: Shiriki Uchanguzi 2025

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals