[Latest Updates]: Kamati ya Bunge Yaipongeza STAMICO kwa Uwekezaji wa Nishati ya Kupikia ya Rafiki Briquettes

Tarehe : March 13, 2025, 1:18 a.m.
left

Kamati ya NISHATI na MADINI wakiongozwa na Mwenyekiti  Mh. Dkt.David Mathayo (MB) leo tarehe 13 Machi walifanya ziara kwenye mradi wa kutengeneza nishati mbadala  ya Rafiki Briquettes.

Katika ziara hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO,  Dkt. Venance Mwasse aliwaongoza wajumbe wa kamati kushuhudia shughuli  mbalimbali zinazofanyika katika uzalishaji nishati ya Rafiki Briquettes  zikiwemo 
Uchomaji wa nyama , mahindi ya kuchoma na upikaji wa maharage.

Wajumbe wa Kamati  walipongeza mageuzi na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Shirika katika mgodi wa Kiwira na Rafiki Briquettes kwa ujumla. 

Wajumbe  pia waliridhishwa na maendeleo ya mradi wa nishati safi ya kupikia ya Rafiki Briquette  na kusisitiza nishati hiyo  muhimu iweze kuwafikia  wananchi wengi  ili kuendelee kuunga mkono ajenda ya  upatikanaji wa nishati safi na nafuu kwa Watanzania wote.

Aidha Mheshimiwa Naibu Waziri wa Madini, Dkt Steven Kiruswa  ambae aliambatana na Kamati katika ziara hiyo aliishukuru kamati kwa maoni yao na miongozo mbalimbali wanayoitoa kwa Shirika ambayo imeleta mafanikio makubwa katika mradi wa Rafiki Briquettes kuanzia utafiti wake hadi kwenye uzalishaji.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals