[Latest Updates]: Tanzania, Canada Kushirikiana Maeneo Mbalimbali Sekta ya Madini

Tarehe : May 8, 2023, 11:59 a.m.
left

*Katibu Mkuu Mahimbali asisitiza ushirikiano kuongeza Tija*

*Dar es Salaam*

Imeelezwa kuwa, Serikali ya Tanzania na Canada zimepanga kushirikiana kwenye maeneo mbalimbali yakihusisha shughuli za utafiti wa madini, kujenga uwezo wa wataalamu na kushirikiana katika kuhamasisha shughuli za uwekezaji nchini ili kuvutia wawekezaji katika Sekta ya Madini.

Hayo yamebainishwa na Balozi wa Canada nchini Tanzania Kyle Nunas leo Mei 8, 2023 jijini Dar es Salaam alipokutana na kuzungumza na Katibu Mkuu Wizara ya Madini Kheri Mahimbali na Wataalamu kutoka Wizara na Taasisi katika kikao kilicholenga kuzungumzia shughuli za kuendeleza uchimbaji wa madini.

Balozi Nunas ameeleza kuwa, upo uwezekano mkubwa wa nchi ya Canada kushirikiana na Tanzania katika uendelezaji wa Madini ya Kimkakati yanayopatikana nchini ikiwemo kufanya utafiti ili kuiwezesha Tanzania kuzalisha madini hayo kwa wingi na uchimbaji wenye tija na endelevu.

“Madini ya kimkakati yanahitajika kwa wingi kwa sasa duniani kwa ajili ya kutumika katika teknolojia mbalimbali ikiwemo kutengeneza betri za magari ili kuzuia hewa chafu (clean energy), simu za mikononi, kompyuta na kutengeneza mota za magari yanayotumia umeme,” amesema balozi Nunas.

Akizungumza katika kikao hicho, Katibu Mkuu Mahimbali amesema kuwa, ushirikiano wa Tanzania na Canada katika Sekta ya Madini utaongeza tija kwenye uchumi, kuongeza ajira, kuwajengea uwezo watumishi ili kuwezesha watanzania kuzalisha madini hayo kwa wingi ikiwemo bidhaa zinazotokana na madini hayo.

“Tunaomba tuweze kuwa na ushirikiano na Canada katika kutangaza shughuli za uchimbaji madini zinazofanyika hapa nchini, tuendelee kukutana na kuzungumza mara kwa mara ili mchango wa Sekta ya Madini ukue katika uchumi wetu,” amesema Mahimbali.

Pia, Mahimbali amesema kuwa, Tanzania iko tayari kushirikiana na Cananda kuhakikisha Taifa linanufaika na rasilimali madini ikiwemo madini ya kimkakati ili kukuza uchumi.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) Dkt. Mussa Budeba amesema, ushirikiano wa Cananda kupitia taasisi (Geological Survey of Canada) na Tanzania katika utafiti wa kijiolojia ili kubaini upatikanaji wa madini muhimu na ya kimkakati katika maeneo ambayo hayajafanyiwa utafiti nchiini.

 "Ni muhimu sana kubadilishana teknolojia mpya kutoka kwa wenzetu katika utafiti kwa kubadilishana wataalamu kupitia Makubaliano ya mashirikiano (MoU),” amesema Dkt. Budeba .

Naye, Mkurugenzi wa Ukaguzi na Biashara ya Madini Tume ya Madini Venance Kasiki amemueleza balozi Nunas maeneo ya kusaidia Tanzania katika Sekta ya Madini ni pamoja na kusaidia kujenga uwezo watumishi wa Wizara ya Madini kwenye Modeli za Fedha (Financial modeling) na uwezo huo utasaidia katika uchambuzi wa upembuzi yakinifu unaoletwa na wawekezaji kabla ya kutoa leseni za uchimbaji madini.

Tanzania imebarikiwa kuwa na madini mengi ya kimkakati yakihusisha madini ya nikeli, kinywe, rare earth elements, cobalt, chuma na madinini mengine ambayo ndiyo yanahitajika kwa sasa duniani kwa ajili ya kutumika katika teknolojia mbalimbali.

 

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals