[Latest Updates]: Ushiriki wa Pamoja Sekta ya Madini Sabasaba Umeongeza Tija kwa Wateja - Dkt. Mwasse

Tarehe : July 7, 2025, 12:40 p.m.
left

Dar aEs Salaam

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini la Taifa  (STAMICO) Dkt. Venance Mwasse amesema ushiriki wa pamoja  wa  Wizara taasisi zake pamoja na wadau wa  Sekta ya Madini katika banda la shirika hilo umeongeza tija kwa kuwa umewarahishia wageni kupata taarifa zote kwenye mnyororo wa shughuli za madini.

Amebainisha hayo leo Julai 7, 2025 baada ya kutembelea banda hilo ambapo
ameonesha kufurahishwa  na idadi kubwa ya wageni wanaotembelea banda huku wakionesha kufurahia huduma na elimu wanazozipata.

"Ni jambo  la kufurahisha kuona banda limetembelewa na wageni wengi ambao wanapata taarifa kutoka kwa wataalam na watoa huduma mbalimbali," amesema Dkt. Mwasse 

Kufuatia hali hiyo, ametoa wito kwa wananchi  kufika ndani ya banda hilo kutokana na uwepo wa  taarifa za kutosha ikiwemo fursa zilizopo katika Sekta ya madini.

Aidha,  ameweza kukutana na 
wataalam mbalimbali wanaoshiriki maonesho hayo kupitia banda hilo.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals