Tarehe : April 27, 2026, 3:22 p.m.

(Januari – Septemba) wastani wa mchango wa sekta umefikia asilimia 11.9. Mwenendo huu umechangiwa na kuongezeka kwa uwekezaji katika Sekta ya Madini.
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai 2025 hadi Machi 2026, Wizara kupitia Tume ya Madini imetoa leseni 454 za Madini Muhimu na Madini Mkakati yakiwemo madini ya kinywe (271), nickel (136), cobalt (2), lithium (6), heavy mineral sands (11) na rare earth elements (28). Utoaji wa leseni hizi unaendelea kuweka msingi thabiti wa kukuza uwekezaji katika utafutaji na uendelezaji wa madini muhimu na madini mkakati nchini.
Kuhamasisha Uwekezaji na Uongezaji Thamani Madini

Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kusimamia shughuli za uongezaji thamani madini nchini kupitia viwanda sita (6) vya kusafisha dhahabu vilivyopo mikoa ya Dodoma (1), Shinyanga (1), Geita (2), Dar es Salaam (1) na Mwanza (1). Aidha, Wizara inaendelea kuhamasisha ujenzi wa viwanda vya kuyeyusha madini ya Shaba, Nikeli, Bati na Chumvi katika mikoa ya Dodoma, Shinyanga, Kagera, Mbeya, Lindi na Pwani. Sambamba na hilo, Wizara inaendelea kushirikiana na wamiliki wa viwanda vya kusafisha dhahabu ili kupata ithibati ya LBMA kwa ajili ya kuwezesha viwanda hivyo kutambulika katika masoko ya kimataifa.
Mheshimiwa Spika, ili kukidhi mahitaji ya wataalam na uwepo wa teknolojia mahsusi katika mnyororo wa thamani wa madini nchini, Wizara imekamilisha taratibu za kuwapeleka wataalamu masomoni ndani na nje ya nchi katika fani mbalimbali zikiwemo: ukadiriaji wa mashapo (resource estimation); modeli za kifedha (financial modelling); ukaguzi na usimamizi wa rasilimali madini; uthaminishaji wa madini; ukataji wa madini ya vito; utengenezaji wa bidhaa za usonara na uongezaji thamani madini. Katika Mwaka wa Fedha 2025/2026, Wizara imepanga kuwajengea uwezo jumla ya watumishi nane (8) katika maeneo ya ukadiriaji mashapo (resource estimation), modeli za kifedha (financial modelling) na ukaguzi wa fedha (financial auditing) migodini.

uchimbaji wa madini wanaanza uzalishaji mara baada ya kukamilisha taratibu za matakwa ya kisheria.
Mheshimiwa Spika, Wizara itatekeleza Mpango Kazi wa Mazingira wa Sekta ya Madini 2025 – 2030 (Mineral Sector Environmental Action Plan – MSEAP) ambao unazingatia Mpango Kazi wa Taifa wa Usimamizi wa Mazingira (National Environmental Action Plan - NEAP) na DIRA 2050. Lengo kuu la Mpango huu ni kujumuisha kanuni za Mazingira, Jamii na Utawala Bora (Environmental, Social and Governance - ESG) katika upangaji, usimamizi na uangalizi wa udhibiti wa Sekta ya Madini nchini, ili kuhakikisha kuwa maendeleo ya rasilimali madini yanachangia ukuaji wa uchumi endelevu bila kuathiri usalama wa mazingira na ustawi wa jamii. Aidha, shughuli za usimamizi na utunzaji wa mazingira zitasimamiwa kwa kuzingatia Nguzo Na. 3 ya DIRA 2050, Sheria ya Madini Sura 123 na Sheria ya Usimamizi wa Mazingira Sura 191.
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.