[Latest Updates]: Benki Kuu ya Tanzania BoT Yakoshwa na Kiwanda cha Mwanza Metals Refinery

Tarehe : Nov. 26, 2025, 12:32 p.m.
left

Bodi ya Wakurugenzi ya BOT, ikiongozwa na  Bw. Emmanuel M. Tutuba, Gavana na Mwenyekiti wa Bodi hiyo, imetembelea kiwanda cha Mwanza  Precious Metal Refinety (MPMR) kwa lengo la  kuongeza uelewa katika shughuli za kiwanda na kujionea mafanikio ya pamoja na maendeleo ya kiwanda kiujumla.

Kwa upande wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), liliwakilishwa na Dkt. Venance B. Mwasse, Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO ambaye aliongozana na Bw. Deusdedith Magala, Mkurugenzi wa Rasilimali watu na Utawala ambaye pia ni  Katibu wa kiwanda cha MPMR.

Katika ziara hiyo, Dkt. Venance B. Mwasse alieleza chimbuko la mradi wa MPMR pamoja na manufaa yaliyopatikana ambayo ni pamoja na kuiwezesha BOT kufikia malengo yake ya kununua dhahabu. 

Kufuatia kukamilika ziara na wasilisho, Gavana kwa niaba ya Bodi aliridhishwa na kazi inayoendelea kiwandani hapo na alitoa pongezi kwa STAMICO pamoja na uongozi wa MPMR kwa kazi nzuri inayofanyika.

Pia Gavana ametoa rai kwa kiwanda cha MPMR kuongeza jitihada za kupata ithibati ya LBMA pamoja na kuongeza mikakati zaidi ya kupata malighafi, ikiwemo kuwawezesha wachimbaji wadogo kifedha

Awali Bodii ya Ushauri ya Chuo cha  Benki Kuu ya Tanzania (BOT) ilitembelea kiwanda hicho.

Bodi ya Ushauri ya Chuo cha BOT iliambatana na Makamu Mkuu wa Chuo Dkt. Ephraim Mwasanguti  kwa lengo la kujifunza na kujionea jinsi kiwanda kinavyoendesha shughuli zake za uongezaji thamani wa madini ya dhahabu pamoja na fedha kwa viwango vya kimataifa. 

Bodi ilifurahishwa na ziara hiyo  kwa  kuwa imekuwa na manufaa sana  na  wameweza kujifunza na kutoa pongezi kwa kiwanda cha MPMR kwa mafunzo na mapokezi waliyoyapata.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals