Tarehe : Nov. 26, 2025, 12:26 p.m.
Arusha
Wanunuzi wa madini kutoka maeneo mbalimbali nchini wameendelea kujitokeza katika Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) jijini Arusha, wakikagua na kuhakiki ubora wa madini yatakayouzwa katika Mnada wa Tatu wa Madini ya Vito unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba 2025.
Ukaguzi huo ni hatua muhimu inayolenga kuhakikisha uwazi, ushindani na ongezeko la thamani ya madini nchini, kwa kuwa madini yote yatakayopatikana kwenye mnada huo wa kidigitali lazima yakidhi viwango na thamani halisi ya soko.
Mnada huo umeendelea kuvutia wanunuzi wengi wa ndani, jambo linalopanua fursa za kibiashara na kuimarisha mchango wa sekta ya madini katika ukuaji wa uchumi wa taifa.
Aidha, unafungua milango kwa wachimbaji na wauzaji kuongeza wigo wa soko kupitia mfumo wa kisasa na salama wa uuzaji.
Hatua hizi ni sehemu ya jitihada za Serikali kupitia Tume ya Madini kwa kushirikiana na Soko la Bidhaa Tanzania (TMX), kuhakikisha mifumo ya usimamizi na mauzo ya madini inakuwa ya kisasa na yenye tija kwa wananchi na taifa kwa ujumla.
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.