Tarehe : May 2, 2018, 9:34 a.m.
Wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Wizara ya Madini, walioko Makao Makuu Dodoma, wameungana na wenzao duniani kote kuadhimisha sikukuu ya Mei Mosi.
Wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Wizara ya Madini walioko Makao Makuu Dodoma, wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa maadhimisho ya sherehe ya wafanyakazi (Mei Mosi).[/caption]
Katika kuadhimisha sikukuu hiyo muhimu, wafanyakazi hao walishiriki maandamano yaliyoanzia katika viwanja vya bunge na kuhitimishwa katika uwanja wa Jamhuri, ambapo walipokewa na Mgeni Rasmi; Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge.
Pamoja na mambo mengine yaliyofanyika wakati wa sherehe hizo, wafanyakazi bora walipatiwa zawadi na vyeti vya kutambua mchango wao.
Baadhi ya Wafanyakazi bora kutoka Idara mbalimbali za Wizara ya Nishati ni Mwamvita Mkakile kutoka Idara ya Nishati, Margaret Vava (Utawala) na Vera Sikana (Sera na Mipango). Taratibu za kuwapata wafanyakazi bora wengine kutoka Idara zilizosalia zinakamilishwa ili waweze kupatiwa vyeti pamoja na zawadi zao.
Kwa upande wa Wizara ya Madini, wafanyakazi bora ni Happy Ndunguru kutoka Idara ya Utawala ambaye pia ndiye mfanyakazi bora wa Wizara. Wengine ni Eugenia Mashoko (Uhasibu), Godfrey Nyamsenda (Sheria), Zuwena Msuya (Mawasiliano Serikalini), Josephat Mbwambo (Sera na Mipango), Christopher Mwita (TEHAMA), Dorothy Mtweve (Madini), Eric Kwesigabo (Ugavi) na Hassan Ngwandu (Ukaguzi wa Ndani).
Imeandaliwa na:
Veronica Simba, Dodoma
Afisa Habari,
Wizara ya Madini,
Kikuyu Avenue,
P.O Box 422,
40474 Dodoma,
Simu: +255-22-2121606/7, Nukushi: +255-22-2121606,
BaruaPepe: info@madini.go.tz,
Tovuti: madini.go.tz
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.