[Latest Updates]: Tume ya Madini Yatoa Wito wa Uhakliki wa Taarifa za Leseni za Madini

Tarehe : May 26, 2026, 5:05 p.m.
left

Dodoma

Tume ya Madini imewataka wamiliki na waombaji wote wa leseni za utafiti na uchimbaji wa madini nchini kuhakiki taarifa zao za leseni na maombi kabla ya Juni 25, 2026, ili kuboresha mfumo wa usimamizi na utoaji wa leseni za madini nchini.

Kwa mujibu wa tangazo lililotolewa na Tume, zoezi hilo linahusisha wamiliki wa leseni za utafiti, uchimbaji mdogo, wa kati na mkubwa wa madini pamoja na waombaji wa leseni mbalimbali za madini.

Taarifa zinazotakiwa kuhakikiwa ni pamoja na anuani zinazojumuisha sanduku la posta, barua pepe, namba za simu pamoja na jina na namba za simu za msimamizi wa mfumo wa portal.

Vilevile, wahusika wanatakiwa kuwasilisha namba ya mlipa kodi (TIN), nakala ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA) au pasi ya kusafiria, pamoja na nyaraka za kampuni ikiwemo Brela Search au MEMART endapo kutakuwa na mabadiliko ya wakurugenzi.

Aidha, Tume imeeleza kuwa nguvu ya kisheria (Power of Attorney) ya msimamizi wa portal nayo ni miongoni mwa nyaraka muhimu zinazopaswa kuwasilishwa katika zoezi hilo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, uhakiki unaweza kufanyika kupitia Mfumo wa Huduma za Leseni za Madini kwa njia ya mtandao (OMCTP) kupitia tovuti ya portal.madini.go.tz au kwa kuwasilisha taarifa hizo katika ofisi za Tume ya Madini.

Leseni za utafiti pamoja na uchimbaji wa kati na mkubwa zitahudumiwa Makao Makuu ya Tume ya Madini jijini Dodoma, huku leseni za uchimbaji mdogo zikihudumiwa katika Ofisi za Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa zilizopo karibu na maeneo ya shughuli za wachimbaji.

Tume ya Madini imeonya kuwa kushindwa kuhakiki taarifa hizo kutasababisha kuondolewa kwa maombi au leseni zenye upungufu katika mfumo wa usimamizi na utoaji wa leseni za madini.

Akizungumza kupitia tangazo hilo, Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Eng. Ramadhani M. Lwamo, amewasisitiza wadau wa sekta ya madini kutoa ushirikiano katika zoezi hilo muhimu kwa maendeleo ya sekta hiyo nchini.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals