[Latest Updates]: Waziri Biteko Kushiriki Kikao cha Baraza la Uchumi na Jamii Umoja wa Mataifa

Tarehe : March 17, 2022, 1:05 p.m.
left

Waziri wa Madini Dkt. Doto Biteko amekutana na Rais wa Baraza la Uchumi  na Jamii la Umoja wa Mataifa  (ECOSOC), Bw. Collen Kelapile katika kikao kilicholenga kupata maelezo kabla ya kushiriki kikao cha Baraza la Uchumi na Jamii la Umoja wa Mataifa kitakachofanyika tarehe 18 Machi, 2022,  katika Ukumbi wa Umoja wa Mataifa, jijini  New York, Marekani.

Tanzania inashiriki katika kikao hicho ikiwa ni  Mwenyekiti wa Nchi Wazalishaji wa Madini ya Almasi Afrika ( ADPA).

Aidha, kikao hicho kinalenga kujadili namna bora za kutumia rasilimali katika nchi husika kuibua maendeleo jumuishi kwenye jamii ambazo maliasili hizo zinapatikana ili zisaidie kuleta amani na hatimaye kufikiwa maendeleo endelevu.

Kikao hicho kitafanyika chini ya mada  isemayo "Maliasili Jamii yenye Amani na Maendeleo Endelevu: *Mafunzo kutoka kwenye Mchakato wa Kimberley

Wengine wanaoshiriki kikao hicho  katika picha ni pamoja na Waziri wa Madini wa Zimbabwe Wiston Chitando ambaye ni Makam Mwenyekiti wa ADPA, Mratibu wa Kimberly Afrika Bw. Jacob  Thamage na Mwakilishi wa Kudumu Umoja wa Mataifa, Balozi Prof. Kennedy Gastorn.
 

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals