[Latest Updates]: Waziri Kairuki afungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Madini

Tarehe : May 8, 2018, 10:17 a.m.
left

Waziri wa Madini, Angellah Kairuki amezindua mkutano wa baraza la kwanza la  wafanyakazi wa Wizara ya Madini mjini Morogoro wenye lengo la kujadili utendaji kazi na namna ya kukabiliana na changamoto katika sekta ya madini.

Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Madini wakiimba wimbo maarufu wa mshikamano (solidarity forever) kwenye mkutano huo

Katika mkutano huo Waziri Kairuki amewataka watumishi kuelekeza nguvu kwenye kutoa kipaumbele kwenye masuala muhimu kama vile kuendelea kutengeneza sera bora zinazosimamia rasilimali za madini na kuweka mfumo mzuri na ulio bora wa ukusanyaji wa mapato ili sekta ya madini iwe na mchango mkubwa katika Pato la Taifa.

Pia, amewapongeza watumishi kwa ukusanyaji wa maduhuli  hadi kuvuka lengo kwa asilimia 130 ya makusanyo ya lengo  lililokuwa limewekwa kwenye Sekta ya Madini.

Aidha, amewataka watumishi kurekebisha kasoro zilizojitokeza katika utekelezaji wa bajeti ya Mwaka 2017/2018 ili kufanya vizuri kwenye bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019

Aidha amewaasa watumishi wote kuwa waadilifu katika utendaji kazi wa kila siku na kuagiza watumishi wote waelimishwe kuhusu maadili katika utumishi wa umma na wale ambao hawajajaza fomu za maadili kujaza mara moja.

Naye Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko amesema Wizara imebeba matarajio makubwa ya wananchi na kuwataka watumishi kufanya kazi kwa weledi ili kuleta matokeo chanya.

Aidha,  amesema Wizara ya Madini ni miongoni mwa Wizara zinazowajibika kuchangia kwa kiwango kikubwa katika Pato la Taifa.

Sekretarieti ya maandalizi katika mkutano huo.

Waziri Biteko amesisitiza mahusiano mazuri baina ya vyama vya wafanyakazi na waajiri  ili Sekta ya Madini iwe na mchango mkubwa kwenye ukuaji wa uchumi wa nchi.

Masuala yaliyojadiliwa katika mkutano huo ni pamoja na  umuhimu wa baraza la wafanyakazi, muundo wa Wizara ya Madini na maadili katika utumishi wa umma. Masuala mengine  yaliyojadiliwa ni pamoja na  mapitio na utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018, mpango wa bajeti wa mwaka 2018/2019 na marekebisho ya Sheria ya Madini ya mwaka 2017.

Mkutano huo umefanyika leo tarehe 07 Mei, 2018 katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) mjini Morogoro.

Imeandaliwa na:

Greyson Mwase,

Afisa Habari,

Wizara ya Madini,

5 Barabara ya Samora Machel,

S.L.P 2000,

11474 Dar es Salaam,

Simu: +255-22-2121606/7, Nukushi: +255-22-2121606,

Barua Pepe: info@madini.go.tz,                                                                               

Tovuti: madini.go.tz

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals