Tarehe : March 23, 2025, 2:21 a.m.
Arusha
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Madini, Machi 22, 2025, walitembelea Kituo cha Jemolojia Tanzania ( TGC) kilichopo jijini Arusha ikiwa ni sehemu ya Wajumbe hao kujifunza kuhusu shughuli zinazotekelezwa na Kituo hicho.
Katika ziara hiyo, pia walitembelea eneo la mradi wa ujenzi wa Jengo la ghrorofa Nane linalotarajiwa katika Kituo hicho pamoja na kutembelea maeneo mbalimbali ya shughuli za utoaji mafunzo ya uongezaji thamani madini ya vito na miamba yanayotolewa na Kituo hicho.
Akizungumza katika ziara hiyo, Kaimu Mratibu Wa Kituo hicho Ally Maganga alisema kwa sasa Kituo hicho kina jumla ya wanafunzi 110 wanaosoma masomo ya muda mrefu na Sita wanachukua mafunzo ya muda mfupi.
"Tumepiga hatua kwenye uzalishaji wa mapambo kutokana na kupata vifaa vya teknolojia ya juu na ni imani yangu baada ya kukamilika kwa mradi huu Kituo hiki kitapiga hatua zaidi," alisema Maganga.
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.