Tarehe : Aug. 6, 2025, 11:06 a.m.
Dodoma, Agosti 6, 2025
Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Menard Msengi, amewakaribisha wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwekeza katika Sekta ya Madini, akisisitiza kuwa mkoa wa Dodoma umebarikiwa kuwa na madini ya aina mbalimbali yenye fursa kubwa za kiuchumi.
Akizungumza alipotembelea Banda la Tume ya Madini katika Maonesho ya Kilimo ya Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma, Mhandisi Msengi amesema ofisi yake imejipanga kikamilifu kutangaza fursa hizo kwa lengo la kuvutia wawekezaji zaidi.
“Dodoma ni miongoni mwa mikoa yenye utajiri mkubwa wa madini mbalimbali hivyo tunawakaribisha wawekezaji kuja kushirikiana nasi kwa maendeleo ya taifa na wananchi,” amesema Mhandisi Msengi.
Maonesho ya Nane Nane yameendelea kuwa jukwaa muhimu kwa wadau wa sekta mbalimbali, ambapo Tume ya Madini inatumia fursa hiyo kutoa elimu kuhusu fursa za uwekezaji katika Sekta ya Madini.
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.