[Latest Updates]: Mwanza Precious Metals Refinery Yakusanya Zaidi ya Tani 5 za Dhahabu kwa Niaba ya BoT

Tarehe : Sept. 26, 2025, 11:13 a.m.
left

Mwanza

Kiwanda cha kusafisha madini ya dhahabu cha Mwanza Precious Metals Refinery (MPMR) kilichopo jijini Mwanza, kimefanikiwa kukusanya zaidi ya tani tano za dhahabu kwa niaba ya Benki Kuu ya Tanzania (BOT).

Hayo yamesemwa na Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Nyaisara Mgaya, alipokuwa akizungumza na ujumbe kutoka nchini Malawi uliotembelea mkoani humo kwa lengo la kujifunza kuhusu usimamizi na uendeshaji wa biashara ya madini, hususan mfumo wa masoko unaotumika nchini Tanzania.

Mhandisi Mgaya amesema kuwa kiwanda hicho kina uwezo wa kusafisha hadi kilo 960 za dhahabu kwa siku, ingawa kwa sasa kinatumia mashine zenye uwezo wa kusafisha kilo 480 kwa siku, kutokana na upatikanaji wa malighafi.

Katika kikao hicho, kiongozi wa ujumbe kutoka Malawi, ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo ya Biashara za Vikundi nchini humo, Zizwan Khonje, amemshukuru Afisa Madini wa Mkoa wa Mwanza kwa elimu waliyoipata kuhusu mfumo wa biashara na masoko ya madini hapa nchini.

“Tanzania ni mfano wa kuigwa katika ukanda wa Afrika Mashariki kutokana na hatua mbalimbali ilizochukua katika kuboresha Sekta ya Madini, ikiwemo uanzishwaji wa masoko ya madini ya wazi na matumizi ya mifumo ya kidijitali katika usimamizi wa rasilimali hizi,” amesema Khonje.

Awali, ujumbe huo ulipata nafasi ya kutembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, ambako walipokelewa na Katibu Tawala wa Mkoa huo Bw. Balandya Elikana, ambaye aliwakaribisha rasmi mkoani humo.

Ziara hiyo ya ujumbe kutoka Malawi inatarajiwa kuwa chachu ya mabadiliko katika sekta ya madini ya nchi hiyo kwa kuimarisha mifumo ya uwazi, kuongeza mapato ya serikali, na kuwezesha ushirikishwaji wa wachimbaji wadogo kwenye soko la kimataifa la madini.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals