[Latest Updates]: REA Yaridhishwa na Uzalishaji wa Nishati ya Kupikia ya Rafiki Briquttes

Tarehe : Jan. 24, 2026, 4:57 p.m.
left

Mwenyekiti  wa Bodi ya REA afurahishwa na STAMICO   kuendelea kuboresha  Ubora wa Rafiki  Briquettes 
Aelekeza Rafiki Briquettes kusambazwa zaidi kila kona ya Tanzania.
DG REA  aahidi kuendeleza mashirikiano  na STAMICO kwa kusaidia kwenye ujezi wa viwanda vingine vya Rafiki Brequettes 
STAMICO  kufanya uzinduzi wa viwanda viwili na kuanza ujenzi wa Kiwanda cha Geita- Ag MD 

Bodi ya Wakurugenzi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeridhishwa na hatua zinazofanywa na  Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kuhakikisha  upatikanaji  wa Nishati Safi ya kupikia ya Rafiki  Briquettes  pamoja na kuendeleza  kuboresha ubora wa Nishati  hii. Sambamba na hayo  imeridhishwa na  kasi ya kuongeza idadi ya Viwanda vyake kufikia vinne  ambapo viwili vya Kisarawe na Kiwira vikiwa vinafanya kazi kwa uwezo wa kuzalisha tani 20 kwa saa, kingine cha Tabora kikiwa katika hatua ya uzinduzi na Dodoma katika hatua ya usimikaji wa mitambo.

Akiongea baada ya ukaguzi wa Kiwanda cha Nishati Safi cha Rafiki  Briquettes  cha Kisarawe  kinachomilikiwa na STAMICO, Mheshimiwa  Balozi Meja Jenerali  Mstaafu Jacob Kingu, Mwenyekiti wa Bodi ya REA  alisema“Mimi na wenzangu kwenye ziara hii tumefarijika sana kuona jinsi ambavyo wenzetu wa STAMICO  walivyopiga hatua ya kujenga viwanda vya kuzalisha Nishati hii ya Rafiki  Briquettes  ambayo ni mbadala wa matumizi ya  Nishati ambazo sio safi kama Kuni na Mkaa. Tumefarijika kuona mfumo mzima wa uandaaji wa Nishati hii na  hatua amabazo STAMICO  imekuwa ikizichukua kuendelea kuboresha Nishati hii. Kama walivyotuelezea, nishati hii inatokana na vumbi  la Makaa ya Mawe (Coal dust) ambayo wanayapitisha kwenye mchakato wa kupunguza hewa za ukaa pamoja na kupunguza ukali wa uwakaji wake. 

Tumeona kwamba pia wamefanya utaratibu wa kupata uthibitisho wa Ubora kutoka Shirika la Viwango la Taifa yaani TBS pamoja na kuweka mtambo mdogo wa utafiti ambao unaendelea kufanya tafiti mbali mbali  kuhusiana na ubora pamoja na tachnolojia mpya. Tumeridhishwa pia na jinsi ambavyo wameweka utaratibu mzuri wa kuwafikia wateja ingawa nataka kuona wanaongeza kasi ili kuwafikia Watanzania wengi. 

Tunajua ajenda kuu ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2034 Watanzania asilimia 80 wanakuwa wanatumia Nishati Safi"

Katika ziara hiyo Mhe Kingu aliambatana na Mha Hassan Saidy,  Mkurugenzi  Mkuu  wa REA,  Mha Sophia Mgonja, Mjumbe wa Bodi, Bwn Stephen Mwakifamba, Mjumbe wa Bodi pamoja na viongozi na watumishi kadhaa kutoka REA. Lengo kuu la ziara hii ilikuwa kukagua kiwanda cha Rafiki Brequettes Kisarawe kuona shughuli nzima ya uzalishaji na ubora wa bidhaa unavyosimamiwa katika uzalishaji na pia kupata picha ya Kiwanda kipya ambacho REA wametoa ufadhili wa TZS Billioni tatu ambacho kitajengwa Geita. 

Naye Mha Hassan Saidy, Mkurugenzi  Mkuu wa REA  ameitaka STAMICO  kuangalia jinsi ya kuwafikia wananchi wengi kwa kuangalia wanavyoweza kushirikiana na Taasisi nyingine za binafsi ili kutekeleza kwa vitendo lengo kuu la kufikisha Nishati hii nchi nzima 

 Aidha alisema ili kufanikisha adhma ya kuifikisha Nishati Safi  nchi nzima  STAMICO  haina budi kuangalia jinsi ya kushirikiana na taasisi nyingine binafsi ambazo  zinaweza kusaidia kusambaza Nishati hii kwa kasi. Aliongeza kuwa  REA ipo tayari kutoa ruzuku kwa Taasisi  ambazo zinatengeneza majiko banifu ili wananchi wengi waweze kuyanunua na kuweza kutumia Nishati ya Rafiki  Briquettes  kwa ufanisi. 

Alisema tayari REA wameshawapa STAMICO  ufadhili kwa ajili ya kiwanda cha Geita na sasa wapo tayari  kutoa ufadhili kwa Kiwanda kingine cha Tanga.

Awali akiwakaribisha na   kuwasilisha taarifa ya mradi huu, Mha Baraka Manyama, Kaimu Mkurugenzi  Mtendaji wa STAMICO  aliwaelezea mipango ya Shirika ni kuhakikisha Nishati hii inasambaa nchi nzima.

 Mha Manayma alisema STAMICO inaendesha viwanda viwili vikubwa vya Rafiki Brequettes vya  Kisarawe  na Kiwira na  sasa Shirika lipo mbioni kuzindua Viwanda cha Tabora  na Dodoma ambavyo vinatarajiwa kuanza Uzalishaji  katika Mwezi  Februari.

Aidha ameongeza kuwa ujenzi wa mitambo ya Kiwanda cha Geita umefika asilimia  50 wakati  taratibu za kumpata mkandarasi wa ujenzi wa Kiwanda zikiendelea. Kwa upande wa Masoko, Mha Manyama aliwaeleza kwamba tayari taassi kama Magereza zote 129,  Kambi za JWTZ,JKT, taasisi za elimu kwa maana ya shule na vyuo, hospitali, masoko ya kuchoma nyama, samaki pamoja na watu binafsi wanatumia Nishati hii ya Rafiki Briquettes.

Alisema Shirika limeshafanya majaribio  ya kukausha mazao ya Chai na Tumbaku na yameenda vizuri.Tayari  Wakulima wa Tumbaku wa Tabora wameeomba Nishati hii ipelekwe wanapoanza kuvuna zao hili mwishoni mwa mwezi wa Januari.

Sambamaba na hao pia kampuni kadhaa za Chai zimeshaanza kuagiza Nishati hii kwa ajili ya kukaushia. 

Kwa upande wa masoko ya Kimataifa, Mha Manyama amesema  tayari  Shirika limeshafanya mawawasiliano ya kuwatembelea Jeshi la Magereza la Uganda na wamepanga kuja kutembelea Kiwanda Mwezi huu wa Februari.

Baada ya mazungumzo na mawasilisho  hayo, Mwenyekiti  wa Bodi, Wajumbe  wa Bodi, Menejimenti  na Watumishi  wa REA walionyeshwa ufanishi wa Rafiki Briquettes  kwa kuonyeshwa inavyochoma nyama, kuchemsha vyakula vigumu kama Makande, Kuchemsha Mahindi, kuonyeshwa vitu vya kukaanga kama Chips na  Kuku  pamoja na kuona mifumo ya majiko ambayo inaifanya Rafiki Briquettes  iwe na ufanisi zaidi.

Viongozi hawa na Watumishi wa REA walifurahia chakula ambacho kiliandaliwa kwa kutumia Nishati hii ya Rafiki Briquettes. 

Mhe Kingu aliwashuku STAMICO  kwa makaribisho mazuri  na kukiri kuwa Nishati hii ina nafasi nzuri ya kuwafikia watu wengi kutokana na gharama zake kuwa za kawaida. Alisisitiza STAMICO  kuongeza kasi ya kuisambaza nchi nzima.

STAMICO  Imejipanga kuendelea kuwa kinara wa kuhakikisha inashiriki kikamilifu katika kuzalisha Nishati hii safi  ya Rafiki  Briquettes ili kufikia lengo la kufikia asilimia 80 ya matumizi ya Nishati Safi ifikapo Mwaka  2034

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals