[Latest Updates]: Tanzania Yataka Msimamo wa Pamoja Kulinda Soko la Almasi Asilia

Tarehe : May 20, 2026, 5:35 p.m.
left

Dkt. Kiruswa aibainisha athari za Almasi za Maabara

Freetown, nchini Sierra Leone

Tanzania imezitaka nchi Wanachama Zinazozalisha Almasi Afrika (ADPA) kuweka msimamo wa pamoja katika kulinda soko la almasi asilia dhidi ya ongezeko la almasi zinazotengenezwa maabara ambazo zimeendelea kuathiri thamani na uaminifu wa soko la madini hayo duniani.

 Wito huo ulitolewa Mei 20, 2026 na Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, wakati akizungumza katika Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa nchi wanachama wa ADPA uliofanyika mjini Freetown, nchini Sierra Leone, ambapo viongozi hao walijadili masuala mbalimbali ya maendeleo ya sekta ya almasi Barani Afrika pamoja na changamoto zinazoikabili sekta hiyo duniani.

Dkt. Kiruswa alisema umuhimu wa kuweka mikakati madhubuti ya mawasiliano na masoko ili kuongeza uelewa kwa walaji kuhusu tofauti kati ya almasi asilia na almasi zinazotengenezwa maabara sambamba na kulinda uhalisia, thamani na mchango wa almasi asilia katika uchumi wa nchi zinazozalisha madini hayo.

Vilevile, alisitiza umuhimu wa nchi za Afrika kushirikiana ili kuwa na mikakati ya pamoja ya kuhakikisha madini yanaongezwa thamani ndani ya bara la Afrika ili kupata manufaa zaidi kutokana na uwepo wa rasilimali hizo katika nchi za Afrika.

Mkutano huo ulipitisha mapendekezo mbalimbali ikiwemo kuimarisha matumizi sahihi ya sifa za kimataifa zitakazotofautisha wazi almasi asilia na zile za sintetiki, pamoja na kuhamasisha taasisi za kimataifa za biashara ya almasi kuunga mkono juhudi hizo kwa manufaa ya sekta ya almasi barani Afrika.

Aidha, nchi hizo zilikubaliana kuimarisha umoja huo ili kukabiliana na changamoto za Biashara ya Almasi duniani.

*#InvestInTanzania *#MIningSector*
*#MineralForGrowth*

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals