[Latest Updates]: TGC Yaendelea Kutekeleza Sheria ya Madini kwa Maslahi ya Taifa

Tarehe : March 21, 2024, 1:19 p.m.
left

●Kuongeza wataalam wa uongezaji thamani madini

● Kuongeza idadi ya  viwanda vya uongezaji thamani madini nchini
● Kuanzisha maabara za Madini ya Vito katika Mikoa yenye Madini

Na.Samwel Mtuwa - Arusha

KATIKA Kutekeleza Sheria ya Madini ya mwaka 2010 na marekebisho yake ya 2017 inayozuia madini ghafi kusafirishwa nje ya nchi, Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) kimejipanga kuhakikisha Sekta ya Madini inaendelea kuimarika kwa uongezaji thamani madini ndani ya nchi ili kuendelea kuleta faida zaidi.

Hayo yamebainishwa leo Machi 21, 2024 na Kaimu Mratibu wa Kituo hicho Mha. Ally Maganga wakati akizungumza na waandishi wa habari waliopo katika ziara ya kutembelea miradi ya Kituo hicho kilichopo  jijini Arusha.

Maganga amesema kuwa ili kufanikisha hilo, kituo cha TGC  kinaendelea kupanua wigo wa utoaji  mafunzo ya uongezaji thamani madini ili  kuwepo na vituo na viwanda vingi vya uongezaji thamani nchini.

Maganga ameeleza  kuwa kitaalam madini yaliyoongezewa thamani yana bei mara dufu ukilinganisha na madini ghafi hivyo  lengo la Sheria hiyo ni kuhamasisha ujenzi na uanzishaji wa viwanda vya uongezaji thamani madini nchini  jambo ambalo TGC imejipanga kutekeleza ili  kuongeza fursa za ajira  kwa vijana pamoja na kuleta fedha za kigeni nchini kupitia mauzo ya madini yaliyoongezewa thamani nje ya nchi.

“Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 na marekebisho yake ya Mwaka 2017  hairuhusu kusafirisha Madini ghafi nje ya nchi, hii ni kwasababu yanakwenda kutengeneza ajira nje, lakini kwa upande mwingine Sheria hii inachochea ajira nchini kwani kuna vijana wanapata ajira hapa kwenye Kituo chetu, kwenye taasisi nyingine za Serikali na nje ya Kituo na wengine wanapata fursa  kwenye viwanda ambavyo vinachakata madini hayo,” amesema Maganga.

Maganga amefafanua mkakati mwingine ni kuwapeleka vijana katika nchi  ambazo Wizara ina mashirikiano ya kikazi ikiwemo Thailand ili kuwapa  utaalam  na uzoefu zaidi katika mnyororo mzima  wa uongezaji thamani Madini.

Maganga aliendelea kusema kuwa Eneo mahsusi ambalo Kituo pia kimejipanga kulitekeleza kikamilifu ni kufungua maabara za Madini ya Vito na metali za thamani kwenye maeneo yenye SHUGHULI za Madini ikiwemo Dar es salaam Ili kurahisisha, kuongeza  tija na kuwahakikishia wananchi thamani halisi ya bidhaa wanazonunua.

Mikakati mingine ni pamoja na ujenzi wa jengo la kisasa litakalo kuwa na  ghorofa nane (8), kutanua wigo wa kutoa huduma za maabara, kuanzisha makumbusho ya madini ya vito na kitengo cha  utafiti wa Madini ya Vito.

 

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals