[Latest Updates]: Nishati Safi ya Rafiki Briquettes Yawa Mkombozi kwa Wakulima na Wafanyakazi

Tarehe : Aug. 4, 2025, 11:02 a.m.
left

Inadumu zaidi ya masaa matatu

Rafiki kwa mazingira

Rafiki wa bei 

Dodoma

Katika mwendelezo wa kuwahimiza na kuhamasisha watanzania katika kutumia Nishati safi ya Rafiki Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) imetumia maonesho ya Nanenane yanayoendelea jijini Dodoma kutoa elimu ya  matumizi ya  nishati safi  ya Rafiki Briquettes.

Akiongea  wakati wa kutoa elimu katika banda la STAMICO, Meneja Masoko na Uhusiano Bw. Deus Alex amezungumzia azma ya  kuhakikisha kuwa nishati hii inawafikia watu wengi ili kuweza kupunguza matumizi ya Kuni na Mkaa unaotokana na Miti. 

Ameongeza pia, katika maonesho hayo STAMICO imeleta bidhaa za kokoto kwa ajili ya Watanzania wanaohitaji kwa ajili ya ujenzi mkubwa na mdogo. Uzalishaji huo wa Kokoto unapatikana eneo la Chigongwe barabara ya Singida.

Akielezea kuhusu nishati hiyo, Deus amefafanua kuwa nishati hii utokana na mabaki ya makaa ya mawe yanayochimbwa katika mgodi wa Kabulo - Kiwira mkoani Songwe ambapo mabaki hayo hupitia mchakato wa kiwandani kupunguza joto na  kuondoa hewa zisizo rafiki kwa matumizi ya nyumbani.

Sambamba na  mradi huo, Deus ametoa  mwaliko kwa wachimbaji wadogo kutembelea maonesho  hayo ili waweze kupata elimu na huduma zinaozohusiana na uchimbaji ndani ya mabanda ya Wizara ya Madini.

Kupitia STAMICO, Serikali mpaka sasa imenunua mitambo 15 Kwa ajili ya kuwahudumia wachimbaji wadogo ili kuwaongezea tija katika shughuli za uchimbaji wa Madini nchini. 

Aidha, Mwenyekiti wa Wanawake na Samia Mkoa wa Dodoma amewaita washiriki wote na watanzania kwa ujumla kufika katika kontena lililopo eneo la manispaa ya zamani ya Dodoma, sabasaba ili waweze kujipatia huduma ya Nishati Safi ya Rafiki Briquettes. 

Kwa upande  wa Taasisi ya Foundation for Disalities Hope Bi. Elizabeth Bundala ametoa rai kwa watanzania wote kutembelea mabanda yaliyo chini ya Wizara ya Madini kujipatia taarifa za mnyororo wa thamani madini.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals