Tarehe : June 23, 2025, 2:03 p.m.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini ahimiza ubunifu, weledi kwa watumishi
Atembelea Banda la Tume ya Madini Katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma
Dodoma, Juni 23, 2025
KATIBU Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Ramadhani Lwamo, na Mkurugenzi wa Rasilimaliwatu na Utawala, Nsajigwa Kabigi, wametembelea banda la Tume ya Madini katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayohitimishwa leo katika viwanja vya Chinangali, jijini Dodoma.
Katika ziara hiyo, viongozi hao wamejionea namna Tume ya Madini inavyoshiriki kikamilifu katika utoaji wa elimu kwa umma kuhusu majukumu yake, huduma mbalimbali zinazotolewa na mafanikio yaliyopatikana katika usimamizi wa rasilimali za madini nchini.
Mhandisi Lwamo sambamba na kuwapongeza wataalam waliopo kwenye banda hilo, amewataka kuendelea kutoa huduma kwa weledi, uwazi na ubunifu kwa kuzingatia mabadiliko ya kidijitali ili kuwawezesha wananchi kupata taarifa kwa haraka na kwa usahihi.
Kaulimbiu ya mwaka huu ni: “Himiza Matumizi ya Mifumo ya Kidijitali ili Kuongeza Upatikanaji wa Taarifa na Kuchagiza Uwajibikaji”, ambayo inalenga kuimarisha utendaji katika utumishi wa umma kupitia matumizi ya teknolojia.
Maadhimisho haya yanahitimishwa leo na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), ambapo taasisi mbalimbali za serikali zimepata fursa ya kuonesha huduma wanazotoa na jinsi zinavyowahudumia wananchi kwa uwazi, uwajibikaji na ubunifu.
Tume ya Madini imeendelea kuwa taasisi muhimu katika kukuza uchumi wa nchi kupitia usimamizi endelevu wa Sekta ya Madini, huku ikiendelea kuboresha huduma kwa kutumia mifumo ya kidijitali kwa maendeleo jumuishi ya Taifa.
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.