Tarehe : Oct. 16, 2025, 12:56 p.m.
Tume ya Madini inaendelea na kikao kazi cha menejimenti jijini Tanga chenye lengo la kutathmini utekelezaji wa majukumu yake na kuweka mikakati mipya ya kuimarisha Sekta ya Madini nchini.
Kikao hicho kinahusisha Makamishna wa Tume ya Madini, Mhandisi Theonestina Mwasha na Dkt. Theresia Numbi, Katibu Mtendaji wa Tume, Mhandisi Ramadhani Lwamo, Wakurugenzi, Mameneja pamoja na Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa.
Kupitia kikao hicho, washiriki wanajadili kwa kina njia bora za kuongeza mchango wa Sekta ya Madini katika Pato la Taifa, ikiwemo kuimarisha usimamizi, kuongeza thamani ya madini nchini, na kuhamasisha uwekezaji endelevu katika sekta hiyo.
Tume ya Madini imeendelea kuwa chachu ya maendeleo katika Sekta ya Madini kupitia usimamizi madhubuti, utoaji wa leseni, elimu kwa wachimbaji, na ufuatiliaji wa shughuli za madini katika ngazi zote za uzalishaji.
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.