[Latest Updates]: Tume ya Madini Yasisitiza Elimu ya Local Content na Utekelezaji wa CSR

Tarehe : Nov. 20, 2025, 1:47 p.m.
left

Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Ramadhani Lwamo, ametoa wito kwa Waratibu wa Local Content na CSR nchini kuimarisha elimu na usimamizi wa kanuni hizo katika ngazi zote za mikoa ili kuhakikisha Watanzania wananufaika kikamilifu na rasilimali za madini.

Mhandisi Lwamo amesema kuwa elimu ndiyo nguzo muhimu inayowasaidia wananchi kuchangamkia fursa za ajira, biashara na huduma ndani ya sekta ya madini, hasa katika kipindi hiki ambacho kampuni zinazomilikiwa na Watanzania kwa asilimia 100 zinatakiwa kutoa bidhaa na huduma mbalimbali kulingana na orodha iliyowekwa.

Ameongeza kuwa Waratibu wa Local Content na CSR wanapaswa kuwa viungo imara kati ya Makao Makuu ya Tume na Ofisi za Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa ili kuhakikisha utekelezaji wa kanuni unafanyika kwa uwazi, umakini na ufanisi.

Sekta ya madini inaendelea kukua kwa kasi na mchango wake kufikia asilimia 10 ya Pato la Taifa, hivyo ni wajibu wa wadau wote kuhakikisha ukuaji huo unaleta manufaa makubwa kwa Watanzania.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals