[Latest Updates]: Eng Samamba Awataka Wadau wa Sekta ya Madini Kutumia Maonesho ya Geita Kuelimisha Wananchi

Tarehe : Sept. 22, 2025, 11:26 a.m.
left

Geita

Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba, amewataka wadau wa Sekta ya Madini kutumia vyema fursa ya Maonesho ya Kimataifa ya Teknolojia ya Madini Geita yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan Bombamlbili kwa kutoa elimu kwa wananchi juu ya mambo muhimu ya sekta hiyo.

Akizungumza mara baada ya kutembelea mabanda ya Wizara ya Madini, taasisi zake na wadau mbalimbali, Mhandisi Samamba amesema maonesho hayo si tu jukwaa la kuonesha bidhaa na teknolojia, bali pia ni sehemu ya kuwafikia wananchi kwa elimu na taarifa sahihi zinazohusu sekta ya madini.

“Wananchi wakielimishwa vizuri watashiriki kwa uelewa, watafaidika zaidi na rasilimali hizi na kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kusimamia sekta hii,” amesema Samamba.

Aidha, Mhandisi Samamba amewapongeza washiriki wote kwa ushiriki wao na kuwasisitiza kuendelea kuonesha nafasi ya Sekta ya Madini katika kuchochea maendeleo ya uchumi wa Taifa na maisha ya Watanzania.

Pia, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Madini Msafiri Mbibo ametembelea mabanda hayo na kupata maelezo kutoka kwa wadau mbalimbali wa madini, maonesho hayo yanatarajiwa kufunguliwa hivi punde na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals