[Latest Updates]: Kamishna wa Madini Awasilisha Mada Katika Kikao cha Utangulizi Kuelekea Mkutano wa 62 wa Bodi ya Kimataifa EITI

Tarehe : March 12, 2025, 1:23 a.m.
left

Madini Mkakati ‘’Critical Minerals”

ARUSHA

Kamishna wa Madini Dkt. Abdulrahman Mwanga leo tarehe 12 Machi, 2025 ameshiriki kikao cha utangulizi cha Bodi ya  Kimataifa ya EITI kilichojadili  masuala ya Madini Mkakati.

Kikao hicho  kimehudhuriwa na wajumbe mbalimbali kutoka kwenye umoja wa nchi wanachama wa Kimataifa EITI. 

Lengo la kikao hicho ni kuzindua utafiti kuhusu Madini Mkakati na hatari za Rushwa zinazoweza kujitokeza katika uvunaji wa Madini hayo. 

Aidha,kikao hicho kimejadili suluhisho la kisera ili kulinda Madini Mkakati kwa lengo la kuwezesha mhamo wa Nishati (Energy transition)

Akizungumzia katika kikao hicho Dkt. Mwanga alilisitiza kuwa kutokana na uhitaji wa Madini hayo muhimu duniani sambamba na ukuaji wa teknolojia ni vyema kuwepo na mkakati wa uvunaji wa madini hayo muhimu Barani Afrika ambapo mkakati huo utasadia kwa nchi wanachama wa Umoja wa nchi za Afrika kutengeneza mikakati yao inayoendana na mkakati mkubwa wa Dunia.

Amesema, wizara kupitia geological survey of Tanzania (GST) imejipanga kikamilifu kufanya tafiti mbalimbali za madini ikiwemo kutoa ushauri elekezi kupitia wataalumu wake, kudhibiti na kuzuia mianya yote ya rushwa.

Aidha,Kikao hicho  kilihudhuriwa na CPA. Ludovick Utouh mwenyekiti wa Kamati ya TEITI pamoja na Katibu Mtendaji wa TEITI Bi. Mariam Mgaya.

Picha na matukio mbalimbali katika kikao hicho:

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals