[Latest Updates]: GST yaonesha fursa za uwekezaji kwenye madini ya kutengeneza mbolea nchini

Tarehe : Aug. 3, 2025, 12:04 p.m.
left

 Yasisitiza taarifa zitokanazo na tafiti zake zina manufaa katika sekta nyingi 

Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imeeleza wadau kupitia maonesho ya nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma kuwa Tanzania ina utajiri madini kilimo yanayotumika kutengenezea mbolea

Hayo yamebainishwa leo tarehe 03/08/2025 leo na Mjiolojia Mwandamizi kutoka GST ndugu Hamis Ramadhani. Bw. Hamisi alielezea ramani ya Tanzania  inayoonesha uwepo wa madini ya kutengeneza mbolea yanayopatikana katika maeneo mbalimbali nchini. 

 Bw. Hamisi alieleza baadhi ya madini kilimo yanayopatikana nchini Tanzania ni pamoja na Bentonite, Diatomite, Dolomite, Gypsum, Limestone, Kaolin na Phosphate.

Bw. Hamisi alieleza kuwa madini hayo sio tu yanatumika kutengeneza mbolea lakini yapo ambayo yanasaidia kupunguza au kurekebisha kiwango cha tindikali katika udongo na hivyo kuboresha afya ya udongo kwa uzalishaji wenye tija wa mazao. 

 Bw. Hamisi alifafanua kuwa tafiti za madini zinazofanywa na GST hazilengi  kuchochea uwekezaji kwenye Sekta ya Madini tu bali hata sekta nyinginezo kama Kilimo, Maji, Nishati na Ujenzi. 

Bw. Hamisi alitoa wito kwa wadua wote kutumia taarifa zinazotokana na tafiti za madini zinazofanywa na GST ili kuongeza tija katika shughuli za kilimo, utafutaji na uchimbaji maji, shughuli za ujenzi na shughuli za utafutaji, uchimbaji na uchenjuaji madini.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals