Tarehe : Feb. 13, 2026, 10:59 a.m.
Mwenyekiti akoshwa na kazi zinzaofanywa na STAMICO
Aahidi Serikali kuendelea kuwekeza kwenye mradi huu
Wakia 8000 za dhahanu kuzalishwa kufikia June 2026.-Ag MD
Mhe Balozi IGP (Rtd) Simon Sirro, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) ameendelea na ukaguzi wa miradi ya STAMICO ambapo alipata nafasi ya kufika katika Mgodi wa STAMIGOLD unaomilikiwa na STAMICO uliopo wilayani Biharamulo mkoani Kagera. Katika ziara hiyo Mhe Balozi Sirro amesema ameendelea kukoshwa na kazi zinazofanywa na STAMICO) huku akiahidi Serikali kuendelea kuwekeza katika mgodi huo.
Mhe Balozi Sirro alipata wasaa wa kukagua maendeleo ya mgodi na kisha kuzungumza na Menejimenti na watumishi wa mgodi huo ambapo aliwaasa kufanya kazi kwa juhudi na kuongeza uzalishaji ili kuongeza tija zaidi.
Alikiri STAMIGOLD imepiga hatua kubwa tangu ianze Mwaka 2013 ambapo imeweza kujitegemea kwa maana ya kuendesha shughuli zake ikiwemo manunuzi bila kutegemea fedha kutoka Hazina.
Aidha Mhe Balozi Sirro ameiagiza STAMIGOLD kuendelea kujikita kwenye tafiti ili kubaini maeneo yanayofaa kwa uchimbaji na kuweza kupanua wigo wa uwekezaji na kufikia malengo ya kuongeza mapato.
Mhe Balozi Sirro ametumia nafasi hiyo pia kusisitiza nidhamu katika matumizi ya fedha za umma kwa watendaji walioaminiwa na kupewa nafasi mbalimbali za kusimamia na kuendesha mgodi huo.
Naye Bwn Deusdedith Magala, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO, alisema STAMIGOLD tayari imeanza miradi mipya kwenye maeneo matatu ya uchimbaji yanayotarajiwa kuongeza uzalishaji.
Bwn Magala alisema ndani ya miezi minne ijayo, hadi kufikia Juni 2026, mgodi utazalisha wakia za dhahabu 8,000 ambazo zitaisaidia STAMIGOLD kupiga hatua kubwa za kiuchumi.
Alisema pia STAMIGOLD imejipanga kufanya tafiti kwenye leseni ambazo hazijawahi kuguswa ili kuongeza uhai wa mgodi huo kutoka miaka mitano ijayo na kufikia zaidi ya miaka 10.
Naye Bwn Ali Ali Meneja Mkuu wa Mgodi wa STAMIGOLD, alisema mpaka sasa mgodi umeajiri wafanyakazi 613 ambao wanafanya kazi na kutimiza wajibu wao kuongeza mapato ya Mgodi.
Alisema tangu mwaka 2013, STAMIGOLD imechangia kiasi cha Tzs Bilioni 56 serikalini na juhudi zinaendelea kuhakikisha uwekezaji uliofanyika unasaidia watanzania kupata manufaa ya mgodi.
Bwn Ali ameihakikishia Bodi ya Wakurugenzi ya STAMICO kuwa utatuzi wa changamoto zilizopo utachochea kuongezeka kiwango cha uzalishaji kufikia wastani wa kilo 30 za dhahabu kwa Mwezi.
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.