[Latest Updates]: Ujenzi Ofisi za Wizara ya Madini Mtumba Wafikia Asilimia 82

Tarehe : June 4, 2024, 12:19 p.m.
left

-Menejimenti ya Wizara yamtaka mkandarasi wa mradi kuongeza kasi

Ujenzi wa Jengo la ofisi ya Wizara ya Madini katika Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma umefikia asilimia 82 na unatarajiwa kukamilika mwezi Septemba 2024.

Hilo limebainishwa leo Juni 4, 2024 na Meneja wa mradi huo, Mhandisi Peter Mwaisabula kutoka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambaye ni Mkandarasi wakati akielezea maendeleo ya mradi mbele ya Menejimenti ya Wizara ya Madini iliyomtembelea kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Wizara ya Madini, Festus Mbwilo amemtaka mkandarasi huyo kukamilisha ujenzi wa mradi huo kwa wakati.

Aidha, Mbwilo amemtaka mkandarasi kutosita kuwasiliana na Wizara pale wanapokumbana na changamoto yeyote ili kuondoa vikwazo vinavyoweza kuchelewesha kukamilika kwa mradi huo.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals