[Latest Updates]: Leseni 73 za Madini Ambazo Hazijaendelezwa Zafutwa

Tarehe : Nov. 25, 2025, 1:27 p.m.
left

Ni Leseni za Utafiti na Uchimbaji Madini wa Kati.

Ni maelekezo ya Mhe. Rais Samia  kuwezesha Vijana 

Waziri Mavunde aelekeza zielekezwe kwenye Programu ya MBT na wawekezaji walio tayari

Eneo la ekari 741,494 lilihodhiwa bila kufanyiwa kazi


DODOMA

WAZIRI wa Madini Mheshimiwa Anthony Mavunde ameilekeza Tume ya Madini kufuta leseni 73 za uchimbaji wa kati na utafiti wa madini ambazo hazijaendelezwa.

Mhe. Mavunde ametoa maelekezo hayo leo Novemba 25, 2025 wakati akiongea na vyombo ya habari katika ukumbi wa Ofisi za Tume ya Madini mjini Dodoma.

Mhe. Mavunde amesema kuwa , ufutaji wa leseni hizo ni utekelezaji wa maelekezo ya Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. Samia Suluhu Hassan ili kuiwezesha Wizara ya Madini kutekeleza majukumu yake kikamilifu na kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanafikiwa na kuhakikisha rasilimali  madini zinawanufaishaWatanzania na Taifa kwa ujumla.

Mhe. Mavunde ameongeza kuwa, eneo lenye ukubwa wa ekari 741,494 lilihodhiwa bila kufanyiwa uendelezaji wowote , jambo ambalo ni kinyume na Sheria ya Madini , Sura 123.
  
Waziri Mavunde amefafanua kuwa, Leseni zilizofutwa ni pamoja na leseni za utafutaji wa madini 44   na leseni 29 za uchimbaji wa Kati kutokana na  kushindwa kurekebisha makosa yao.

Akielezea kuhusu matumizi ya maeneo yote yaliyofutwa, Mhe. Mavunde amesema kuwa, maeneo hayo yatapangwa kwa ajili ya mradi wa vijana katika programu ya Mining Better Tomorrow (MBT) ili waweze kunufaika na rasilimali madini.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals