[Latest Updates]: Masoko Rasmi, Bei Elekezi Yapunguza Utoroshaji wa Madini Ruvuma

Tarehe : May 24, 2026, 5:17 p.m.
left

Ruvuma

Uanzishwaji wa masoko rasmi ya madini pamoja na matumizi ya mfumo wa bei elekezi mkoani Ruvuma, umetajwa kupunguza kwa kiasi kikubwa vitendo vya utoroshaji wa madini huku ukiongeza mapato ya Serikali na kuwanufaisha wachimbaji wadogo.

Mkoa wa Ruvuma kwa sasa una masoko rasmi ya madini mawili likiwemo Soko la Dhahabu na Vito la Songea Mjini pamoja na Soko la Dhahabu na Vito Tunduru, lililozinduliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan Septemba 26, 2024.

Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Alphonce Bikulamchi, amesema mafanikio hayo yametokana na maboresho yaliyofanywa na Serikali katika usimamizi wa biashara ya madini kupitia masoko rasmi yenye uwazi na ushindani wa kibiashara.

Amesema kabla ya kuanzishwa kwa masoko hayo, baadhi ya wachimbaji walikosa maeneo rasmi ya kuuza madini yao hali iliyochochea biashara holela na utoroshaji wa madini, jambo lililoikosesha Serikali mapato na kuwafanya wachimbaji wadogo kuuza madini yao kwa bei isiyo na tija.

“Kwa sasa wachimbaji wanapata taarifa sahihi za bei elekezi za madini yao, jambo ambalo limeongeza uwazi, kuondoa mianya ya udanganyifu na kuongeza imani katika biashara ya madini,” amesema Mhandisi Bikulamchi.

Ameeleza kuwa uwepo wa wanunuzi kutoka ndani na nje ya nchi katika masoko hayo umeongeza ushindani wa bei na kuwawezesha wachimbaji kuuza madini yao kwa thamani inayostahili.

Aidha, amesema Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya biashara ya madini kwa kuimarisha usimamizi wa masoko na kutoa elimu kwa wachimbaji ili kuhakikisha sekta hiyo inaendelea kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa pamoja na maendeleo ya wananchi.

Kwa mujibu wa Mhandisi Bikulamchi, hatua hiyo pia imeongeza ushiriki wa wachimbaji wadogo katika uchumi rasmi na kusaidia kudhibiti vitendo vya utoroshaji wa madini mkoani Ruvuma.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals