[Latest Updates]: Waziri Kairuki atembelea eneo la Mpaka wa Namanga

Tarehe : Aug. 10, 2018, 6:50 a.m.
left

Na Asteria Muhozya,

Waziri wa Madini Angellah Kairuki, akiongozana na Mkuu wa  Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo , Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Longido pamoja na ujumbe aliombata nao wakati wa ziara yake mkoani Arusha, tarehe 9 Agosti,2018, alitembelea eneo la Mpaka wa Namanga, linalotenganisha nchi ya Tanzania na Kenya.

Waziri wa Madini Angellah Kairuki akimsikiliza Anorld Kisheshi wakati akitoa ufafanuzi wa namna scanner katika eneo hilo zinavyofanya kazi.[/caption]

Waziri Kairuki alitembelea eneo husika kwa lengo la kukagua na kuangalia namna shughuli za udhibiti wa utoroshaji wa madini  maeneo ya mipakani  zinavyoendelea.

Waziri Kairuki alisema baada ya kufika eneo husika alikuta kuna suala la changamoto ya upungufu wa wafanyakazi na hivyo kuahidi kulifanyia kazi kwa haraka suala hilo.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo alisema changamoto katika eneo hilo ni upungufu wa wafanyakazi na kuongeza kuwa, tayari Waziri wa madini ameahidi kulifanyia kazi suala husika ili kudhibiti utoroshaji madini katika maeneo ya mipaka.

Aliongeza kuwa, tayari Serikali ya Wilaya imeanza kuweka alama kujua mipaka ya Tanzania katika eneo husika ikiwemo kufuatilia njia za panya ambazo zinaweza kutumika kutorosha madini nje ya nchi.

Naye Mkaguzi wa Migodi, Anold Kisheshi alisema kuwa, serikali imekuwa ikitumia njia mbalimbali kudhibiti utoroshaji wa madini katika maeneo ya mipaka.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals